Skip to main content

DHIMA YA VIJANA KATIKA KUIMARISHA UCHUMI WA KENYA

 


Hivi karibuni Taifa la Kenya limeingia katika uchumi wa kati ambalo ni jambo muhimu sana katika mtazamo wa kusonga mbele na kuimarisha tena Uchumi wa Taifa hili ambao umelemazwa tangu kuzuka Kwa janga la Covid 19.

Photo cortesy of opera

Kijana ni mwanajeshi wa mstari wa mbele katika vita ya kiuchumi na hivyo ikiwa kijana hata shiriki katika shughuli za kiuchumi ambazo zina wezesha serikali kuu kukusanya mapato,kijana huyo anakuwa ni mwanajeshi atumikaye kulidondosha Taifa lake kiuchumi hasa ikizingatiwa kuwa anazo nguvu za kutumika katika nafasi ya kulisaidia Taifa lake Kenya kukua kiuchumi ivyo akiwa hatumiki ndani ya Taifa kwa shughuli za kiuchumi atakuwa  analemaza uchumi kwa Taifa.


Kijana anapaswa kuzingatia  kuwa kuwa ikiwa kuna kupanda kwa uchumi wa Nchi  pia kuna kushuka kwa uchumi wa Nchi.


Hivyo basi tunapokuwa tungali bado vijana na tuna nguvu ni muhimu kujua kuwa uchumi wa Taifa letu lipo mabegani Mwetu .


Photo cortesy of nation media

Hivyobasi uchumi wa Taifa la Kenya  katika kupanda au kushuka Kwale unategemea nafasi ya vijana ndani ya Taifa hilo


Taifa kupanda kiuchumi ni kazi sana kuliko Taifa kushuka kiuchumi ni raisi sana , ikiwa Taifa la Kenya litapanda kiuchumi sisi vijana wa Taifa hili ni lazima tujiulize je nina nafasi gani ya kuendelea kulisababishia Taifa  kukua kiuchumi zaidi.


Photo cortesy of nation media

Jambo la muhimu kabisa nikuwa vijana ndio nguvu kazi ya kuusogeza uchumi wa Nchi husika kusogea mbele au kurudi nyuma hivyo tunachotakiwa kukifanya  ni kujitoa sana katika Kuhakikisha uchumi wa Taifa letu unaendelea kukua kutoka kiwango vya chini kupelekea juu zaidi na huku tukimtanguliza Mungu kwa kila jambo katika maswala kiuchumi.


MWANDISHI

VINCENT MUTWIRI

Comments

Post a Comment