Skip to main content

Mabadiliko ya tabia nchi na athari zake

 

Tabia ya nchi ni mwenendo wa hali ya hewa yakiwemo majira, wastani na vizio vya juu na chini kabisa vya joto, utokeaji na mtawanyiko wa mawingu, mvua na theluji, majanga yanayosababishwa na hali ya hewa kama vile upepo mkali na kuanguka kwa theluji, na vimbunga vikali vya nchi kavu na baharini. Tabia ya nchi duniani inabadilika kwa sababu ya kile kinachojulikana kama ‘athari zilizoongezwa nguvu za miali ya jua’.

Image Courtesy of google

Uhai unawezekana Duniani kwa sababu ya nishati ya jua ambayo hufika katika umbo la mwanga. Dunia huakisi sehemu ya mwanga huu ambao hatimaye hupotelea angani. Hata hivyo, gesi zilizoko kwenye anga hupunguza kasi ya kupotea huku kwa mwanga. Kwa pamoja, gesi hizi hujulikana kama ‘gesi za kuzuia miali ya jua’, kwa Kiingereza, ‘greenhouse gases’, kwani kazi yake ni kuzuia joto lisipotee Duniani. Hii ni kama inavyoonekana katika nyumba maalumu zilizofunikwa kwa nailoni wanazotumia wakulima ili kuotesha mbogamboga.


Kiasi fulani cha gesi hizi ni muhimu ili kutuwezesha kuishi pasipo gesi hizi, wastani wa joto Duniani ungalikuwa nyuzi joto za 19°! Hata hivyo, shughuli za kiuchumi za binadamu (kama vile kilimo, uendeshaji viwanda, na ukataji miti misituni) zinasababisha gesi hizo za kuzuia miali ya jua kuwa nzito zaidi na kwa hiyo kuongeza athari zaidi za miali ya jua Duniani. Ongezeko la joto kwa kawaida hufuatiwa na mabadiliko katika utokeaji wa mawingu, kiasi cha mvua na theluji inayoanguka, mienendo ya pepo na urefu wa majira. Tayari tumeanza kushuhudia baadhi ya mabadiliko haya.

Photo courtesy of google

Kwa sababu mifumo ya hali ya hewa ina miingiliano mingi ya aina yake, mabadiliko ya hali ya hewa yana maana kwamba baadhi ya maeneo duniani hivi sasa yanapata kiwango cha chini cha joto kuliko kawaida, huku maeneo mengine yakipata kiwango cha juu mno na hata mara nyingine kushuhudia hali ya hewa mbaya kupita kiasi, kama vile kupigwa na vimbunga vikali vya nchi kavu na baharini na kughubikwa na dhoruba.


Mwandishi 

Vincent Mutwiri

Comments

  1. Kazi nzuri kabisaa

    ReplyDelete
  2. ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

    ReplyDelete
  3. Nice work am impressed

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

How to deal with baneful relationships

Relationships are always interesting and fun when they are smooth and it feels very interested when your partner is also your friend. However, if relationship starts becoming toxic between partners and still percevere, it brings an image of slavery and many find it difficult to cope and end in engaiging in acticities that put them into regrets afterwards. No one wants to find themselves in relationships that are full of quarrels, misunderstandings and traumatizing. However, they rather get out of such relationships when it is too late. When someone finds it difficult in relationship especially for the campus students, their natural reaction in such is to avoid dealing with situation. However its good to know how to deal with such toxic relationships  Bellow are some of the reasons why campus students find rough times in their toxic relationships and still tolerate : 1.Viewing toxity as normal Most people get themselves in abusive relationships and not able to know how to cope with ...

HOFU YA EBOLA NCHINI KENYA

 Kufuatia kudhibitishwa kuwepo kwa virusi vya Ebola nchini Uganda mnamo tarehe 19 mwezi wa tisa 2022 , wizara ya afya nchini humo sasa yawataka waadhiriwa licha ya kupokea matibabu, kuepuka tendo la ndoa angalau kwa siku tisini. Haya yanajiri baada ya kubainika kwamba virusi hivi bado vinaenea hata baada ya muadhiriwa kupokea matibabu hivyo basi kusambazwa sio kwa njia ya mate na damu pekee ila wanasayansi sasa wanabaini kuna uwezekano wa virusi hivyo kupatikana kwenye manii (semen) ya mwanaume hata baada ya kupata matibabu dhabiti. Haya yaanjiri baada ya watu 36 kudaiwa kupatikana na virusi hivyo huku wengine 23 kudaiwa kufariki kutokana na makali ya virusi hivyo kulingana na takwimu za serikali ya Uganda. Wizara ya afya nchini Kenya yaonyesha hofu ya virusi hivyo vya Ebola kukurupuka nchini na kuzitaja kaunti 20 zilizo kwenye hatari zikiwemo :Busia, Machakos, Nakuru, Kiambu, Nairobi, Kajiado, Makueni, Taita Taveta, Mombasa, Kwale, Kericho,Bungoma, Trans Nzoia, West Pokot, Turkana...