Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2022

PANDASHUKA KATIKA SAFARI YA UANDISHI WA HABARI KATIKA CHUO KIKUU

 Bilashaka wanasema kila safari huanza na hatua moja na vilevile katika kila hatua hakukosi changamotowe. Chuo kikuu ni mojawapo ya matamanio ya kila mwenye ari ya masomo kufikia ila kupitia vikwazo mbalimbali sio wote hufaulu katika safari hii kwani wengi hulazimika kuachisha safari hii katikati au pia kukosa nafasi kabisa ya kuianza. Fauka ya hayo, binafsi nimefaulu kuanza masomo kwenye ngazi ya stashahada ya uanahabari katika chuo kikuu cha kiufundi cha Mombasa na kufikia sasa nimekamilisha safari hii kwa asilimia 99. Sio kumaanisha kwamba maisha yamekuwa mtelezo ila changamoto zimekuwepo kiasi cha kukatishwa tamaa na maneno ya wanafunzi wenzangu. Picha kwa hisani ya Okwonko Dhana iliyopo kwa wengi walio nje ya masomo ya vyuo vikuu ni kwamba kila mwenye kufika katika chuo kikuu kwa ngazi yoyote, ni mtu mzima na kwa njia moja au nyingine ana uwezo wa kjisimamia kwenye matumizi yake ya kifedha bila ya kumtegemea mtu yeyote wakiwemo wazazi. Ni vigumu kuamini ila katika kuju

DHIMA YA VIJANA KATIKA KUIMARISHA UCHUMI WA KENYA

  Hivi karibuni Taifa la Kenya limeingia katika uchumi wa kati ambalo ni jambo muhimu sana katika mtazamo wa kusonga mbele na kuimarisha tena Uchumi wa Taifa hili ambao umelemazwa tangu kuzuka Kwa janga la Covid 19. Photo cortesy of opera Kijana ni mwanajeshi wa mstari wa mbele katika vita ya kiuchumi na hivyo ikiwa kijana hata shiriki katika shughuli za kiuchumi ambazo zina wezesha serikali kuu kukusanya mapato,kijana huyo anakuwa ni mwanajeshi atumikaye kulidondosha Taifa lake kiuchumi hasa ikizingatiwa kuwa anazo nguvu za kutumika katika nafasi ya kulisaidia Taifa lake Kenya kukua kiuchumi ivyo akiwa hatumiki ndani ya Taifa kwa shughuli za kiuchumi atakuwa  analemaza uchumi kwa Taifa. Kijana anapaswa kuzingatia  kuwa kuwa ikiwa kuna kupanda kwa uchumi wa Nchi  pia kuna kushuka kwa uchumi wa Nchi. Hivyo basi tunapokuwa tungali bado vijana na tuna nguvu ni muhimu kujua kuwa uchumi wa Taifa letu lipo mabegani Mwetu . Photo cortesy of nation media Hivyobasi uchumi wa Taifa la Kenya  kat